SUAMEDIA

SACIDS - SUA kutoa mafunzo Mozambique namna ya kutumia Mfumo wa Afya Data

 Na Gladness Mafuru

Imeelezwa kuwa mfumo wa Afya data hivi sasa umeanza kutumiwa na nchi jirani kama Mozambique wakishirikiana na Wakfu wa Utafiti na Udhibiti wa Magonjwa Ambukizi ya afya moja wa SACIDS kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA.

Picha kutoka Maktaba


Hayo yameelezwa na Afisa Mawasiliano wa SACIDS Yunus Karsan April 28,2021 wakati akizungumza na SUAMEDIA ofisini kwake.

Karsan amesema hivi sasa tayari timu ya SACIDS kutoka SUA ipo Mozambique kwa ajili ya kutoa mafunzo ya namna ya kutumia mfumo wa Afya Data katika kukusanya taarifa za magonjwa kutoka  kwa jamii  wanyama na binadamu.

Ameongeza kuwa mfumo huo wa Afya Data una wigo mpana wa kutumika  ulimwenguni kutokana na kuwa unaweza kubadili lugha kutokana na mahitaji ya eneo husika.

Aidha ametoa wito kwa wanafunzi wa SUA kwa ngazi za Uzamili na Uzamivu kujitokeza kwenye nafasi za kwenda kusoma nje ya nchi pamoja na kufanya tafiti  katika vyuo washirika kama vile NSG iliyopo South Afrika, Uingereza na Korea.

Post a Comment

0 Comments