SUAMEDIA

Waziri Mwambe: Hayati Magufuli alikuwa na mtazamo mpana kiuchumi

 

Na: Farida Mkongwe

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Geoffrey Mwambe amemuelezea Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kuwa ni Kiongozi aliyekuwa na mtazamo mpana kiuchumi na ndio maana Nchi  ya Tanzania iliingia mapema kwenye uchumi wa kati.

Picha  na Star and Stripes


Mhe. Mwambe ameyasema hayo mapema leo asubuhi Machi 25,2021  kupitia Azam TV wakati akizungumza kwenye Viwanja vya Magufuli wilayani Chato kabla ya wananchi hawajaanza kutoa heshima zao za mwisho kwa Hayati Magufuli.

Waziri Mwambe amesema ana imani kupitia uongozi wa Rais wa sasa Mhe. Samia Suluhu Hassan na mipango yote ya Serikali kuhusu suala la viwanda itazidi kusonga mbele kwa kuwa Mama Samia alikuwa akishirikiana kwa karibu na Hayati Magufuli.

Amesema wananchi hawana sababu ya kuwa na wasiwasi kwa kuwa Rais Samia Suluhu Hassan ataendelea kuyasimamia, kuyaenzi na kuongoza kama ambavyo alikuwa akifanya Hayati Dkt. Magufuli.

Kuhusu suala la kuyaendeleza masoko na wajasiriamali, Mh. Mwambe amesema tayari ameshatoa maelekezo kwa Taasisi ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzanai TAN-TRADE kuongeza juhudi za kimkakati kuhakikisha masoko yaliyofunguliwa yakiwemo ya Afrika Mashariki yanaendelezwa ipasavyo.

                                                        -30-

Post a Comment

0 Comments