SUAMEDIA

Mkuu wa Upelelezi Ilala Afariki kwa Ajali


Mkuu wa upelelezi Mkoa wa Kipolisi Ilala, Aanael Mbise (50) na Frank Macha (35) mkazi wa Dar es Salaam ambaye ni fundi umeme wamefariki dunia na mmoja kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuacha njia na kugongana na gari jingine mkoani Kilimanjaro.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Hamisi Issah amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo iliyotokea Jana eneo la Kiverenge Wilaya ya Mwanga.

Issah amesema ajali hiyo imehusisha gari aina ya Toyota Prado iliyokuwa ikitokea Same kuelekea Moshi na basi dogo la kampuni ya KVC iliyokuwa ikitokea Moshi kuelekea Same..Amemtaja aliyejeruhiwa katika ajali hiyo kuwa ni Samson Macha (23) ambaye ni Mkazi wa Dar es salaam na amevunjika mguu wa kushoto na anaendelea kupatiwa matibabu Hospitali ya Wilaya ya Same akisaidiwa na ndugu yake Daniel Macha.


Post a Comment

0 Comments