TIMU ZA KIKAPU ZITOE HAMASA KWA WATOTO KUCHEZA MCHEZO HUO
Na Alfred Lukonge
Wito
umetolewa kwa timu za mpira wa kikapu hapa nchini kuhamasisha watoto wadogo
kujifunza mchezo huo hasa wale wa shule za msingi ili kukuza maendeleo ya
mchezo huo kwa miaka ya baadae.
MOHAMED YUSUPH WA KWANZA KUSHOTO AKIWA NA WACHEZAJI WENZIE WA SAVIO
Wito
huo umetolewa na mchezaji wa mchezo huo ambaye pia ni mkufunzi kutoka timu ya Savio Mohamed Yusufu alipozungumza
na SUAMEDIA.
“nathamini sana maendeleo ya mchezo wa mpira
wa kikapu hapa nchini ndio maana nimeanzisha programu mahususi kwa watoto
wadogo kila siku ya Jumamosi kuanzia saa mbili na nusu asubuhi mpaka saa sita
na nusu mchana katika viwanja vya Don Bosco Upanga”.alisema Yusufu.
Pamoja
na hayo Yusufu aliwataka waandishi wa habari za michezo hapa nchini kuacha
kuupa kipaumbele mchezo wa soka pekee na kuangalia michezo mingine, jambo
ambalo kwa upande wake anaona itakuwa ni njia mojawapo ya kukuza michezo
mingine pamoja na kuiongezea mashabiki.
Yusufu alianza kucheza mpira wa kikapu mwaka
1996 kipindi akiwa darasa la sita katika shule ya msingi Muhhimbili baada ya
kuvutiwa na wachezaji nguli wa timu hiyo Peter Bategeki na Dorii Nima na ndoto
zake ni kucheza mashindano ya dunia ya mpira wa kikapu.
YANGA KUKUBALI KICHAPO 3-1
Na: Fadhila
Kizigo
Michuano
ya Kombe la Shirikisho Afrika kati ya Tp Mazembe dhidi ya Yanga umemalizika kwa
Yanga kukubali kipigo cha magoli 3-1 ikiwa ugenini DRC.
Mshambuliaji
Bolingi wa Tp Mazembe aliifungia timu yake goli la kwanza kipindi cha kwanza
dakika ya 28 na hadi kipindi cha kwanza kuisha Yanga bila kurudisha goli.
Kipindi
cha pili katika dakika ya 11 Rainford Kalaba aliifungia Tp Mazembe goli la pili
kabla ya kuifungia goli la tatu mnamo dakika ya 64.
Katika kipindi
hichphichp cha pili cha mchezo Hamis Tambwe aliiandikia goli pekee la Yanga na
hadi mchezo ulipomalizika TP Mazembe 3 na Yanga 1 na hivyo Tp Mazembe imepata nafasi ya kuongoza kundi A kwa pointi
13 ikifuatiwa na Bejaia yenye pointi 8.
NDANDA KUMINYANA NA MWADUI YA SHINYANGA LEO
TIMU ZA KIKAPU ZITOE HAMASA KWA WATOTO KUCHEZA MCHEZO HUO
Na Alfred Lukonge
Wito umetolewa kwa timu za mpira wa kikapu hapa nchini kuhamasisha watoto wadogo kujifunza mchezo huo hasa wale wa shule za msingi ili kukuza maendeleo ya mchezo huo kwa miaka ya baadae.
Wito umetolewa kwa timu za mpira wa kikapu hapa nchini kuhamasisha watoto wadogo kujifunza mchezo huo hasa wale wa shule za msingi ili kukuza maendeleo ya mchezo huo kwa miaka ya baadae.
MOHAMED YUSUPH WA KWANZA KUSHOTO AKIWA NA WACHEZAJI WENZIE WA SAVIO |
Wito huo umetolewa na mchezaji wa mchezo huo ambaye pia ni mkufunzi kutoka timu ya Savio Mohamed Yusufu alipozungumza na SUAMEDIA.
“nathamini sana maendeleo ya mchezo wa mpira
wa kikapu hapa nchini ndio maana nimeanzisha programu mahususi kwa watoto
wadogo kila siku ya Jumamosi kuanzia saa mbili na nusu asubuhi mpaka saa sita
na nusu mchana katika viwanja vya Don Bosco Upanga”.alisema Yusufu.
Pamoja
na hayo Yusufu aliwataka waandishi wa habari za michezo hapa nchini kuacha
kuupa kipaumbele mchezo wa soka pekee na kuangalia michezo mingine, jambo
ambalo kwa upande wake anaona itakuwa ni njia mojawapo ya kukuza michezo
mingine pamoja na kuiongezea mashabiki.
Yusufu alianza kucheza mpira wa kikapu mwaka
1996 kipindi akiwa darasa la sita katika shule ya msingi Muhhimbili baada ya
kuvutiwa na wachezaji nguli wa timu hiyo Peter Bategeki na Dorii Nima na ndoto
zake ni kucheza mashindano ya dunia ya mpira wa kikapu.
YANGA KUKUBALI KICHAPO 3-1
YANGA KUKUBALI KICHAPO 3-1
Na: Fadhila
Kizigo
Michuano
ya Kombe la Shirikisho Afrika kati ya Tp Mazembe dhidi ya Yanga umemalizika kwa
Yanga kukubali kipigo cha magoli 3-1 ikiwa ugenini DRC.
Mshambuliaji
Bolingi wa Tp Mazembe aliifungia timu yake goli la kwanza kipindi cha kwanza
dakika ya 28 na hadi kipindi cha kwanza kuisha Yanga bila kurudisha goli.
Kipindi
cha pili katika dakika ya 11 Rainford Kalaba aliifungia Tp Mazembe goli la pili
kabla ya kuifungia goli la tatu mnamo dakika ya 64.
Katika kipindi
hichphichp cha pili cha mchezo Hamis Tambwe aliiandikia goli pekee la Yanga na
hadi mchezo ulipomalizika TP Mazembe 3 na Yanga 1 na hivyo Tp Mazembe imepata nafasi ya kuongoza kundi A kwa pointi
13 ikifuatiwa na Bejaia yenye pointi 8.
NDANDA KUMINYANA NA MWADUI YA SHINYANGA LEO
Ligi Kuu
Tanzania Bara itaendelea
tena leo Jumatano Agosti 24, 2016 kwa kucheza mchezo mmoja, ambapo Toto
Africans ya Mwanza itaikuwa mwenyeji
wa Mwadui FC.
Mwadui FC inacheza
ugenini ikiwa inarekodi nzuri
ya kushinda michezo
mitatu mfululizo ya mwisho
katika ligi kuu
Tanzania bara wakati
Toto Africans ikiwa imeshinda mchezo
mmoja kati ya mitatu ya hivi
karibuni.
Mchezo huo
utachezwa katika dimba
la CCM kirumba
majira ya saa 10:05
kwa saa za
Afrika ya mashariki.
Timu
hizo hazijacheza mchezo
wowote wa msimu mpya wa 2016-2017 wa ligi
kuu Tanzania bara ikiungana
na Yanga SC.
NDANDA YAJIFUA KUIVAA MTIBWA
Na:Adam
Ramadhan
Klabu ya
Ndanda FC imeweka
kambi ya mazoezi ya
siku tano mkoani
Morogoro katika uwanja
wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), kwa ajili
ya kujifua na kujiandaa
na mchezo dhidi
ya Mtibwa Sugar katika
mchezo wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Akizungumza na
SUAMEDIA Afisa Habari
wa Klabu hiyo
Idris Bandali amesema
kuwa kambi hiyo
imeanza jana jumatatu
na itamalizika ijumaa
ya wiki hii, “Mazoezi
haya yatakuwa yanafanyika
asubuhi tu na
tunajipanga ili kufanya
vizuri mara baaada
ya kupoteza mchezo
wa kwanza dhidi ya
Simba, kwa hiyo mashabiki
wa Ndanda FC
watarajie matokeo mazuri
tu dhidi ya Mtibwa
Sugar” alisema Bandali.
Hata hivyo
amesema kuwa lengo
lao kubwa msimu huu
ni kumaliza ligi ikiwa
katika tatu bora na
ikiwezekana kuleta upinzani
mkubwa katika ligi hiyo, kwa kupambana
vilivyo ili kufanya
ligi iwe ya
ushindani.
Ndanda FC
ilipanda daraja msimu
wa mwaka 2014/15
na kumaliza ligi
ikiwa nafasi ya tisa
msimu wa 2015/16, tayari msimu
huu imepoteza mchezo wake
wa kwanza dhidi
ya Simba, na hivyo
jumamosi itacheza na
Mtbwa Sugar kwa jihadi
ilikuata matokeo mazuri.
YANGA KUIVAA MAZEMBE LEO
Na:Adam
Ramadhan
Klabu ya
Yanga leo itakuwa mgeni wa
TP Mazembe Mjini Lubumbashi
Congo DR kucheza mchezo
wao wa kukamilisha
ratiba ya kundi
A katika kombe
la shirikisho Afrika
mchezo utakaochezwa majira
ya saa 9:30 kwa saa
Afrika ya mashariki.
TP Mazembe
wanaongoza kundi hilo
wakiwa na alama
10 wakifuatiwa na
Medeama wenye alama
8,nafasi ya tatu
ikishikwa na MO Bejaia
yenye alama 5 huku klabu
ya Yanga ikiburuza mkia
kwa alama 4.
Kuelekea mchezo
huo Yanga SC itawakosa
baadhi ya wachezaji kutokana
na majeraha na adhabu
ya kadi za
njano, Watakaoukosa mchezo huo kutokana na majeraha ni
Obrey Chirwa, Nadir Haroub, Juma
Abdul na Vincent
Bossou wakati Donald
Ngoma na Kelvin
Yondani wataukosa mchezo huo kutokana
na kadi mbili za
njano.
Ushindi au
sare ya aina
yoyote itaivusha Medeama
kwenda nusu fainali
huku MO Bejaia ikihitaji
angalau goli mbili iweze
kufuzu hatua hiyo ya nusu
fainali .
ELIMU YA SANAA IFUNDISHWE TOKA SHULE ZA AWALI: MWANIKE
Na: Alfred Lukonge
Imeelezwa
kuwa elimu ya sanaa ianze kufundishwa
toka shule za awali kwani kwa kufanya hivyo kunaweza kupelekea Taifa kuwa na
hazina kubwa ya watu wenye vipaji pamoja
na kutengeneza ajira binafsi.
MSANII HILIMALI AKIWA NA NGULI WA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA JUMA KASSIM NATURE |
Hayo
yamesemwa na msanii wa muziki wa kizazi kipya Hilimali Mwanike Waukaya Jumatatu
ya tarehe 21/8/2016 alipozungumza na SUAMEDIA na kubainisha kuwa “sanaa ni kazi
kama kazi zingine hivyo serikali ikitia mkazo kwenye sanaa inaweza kuwa njia
mojawapo ya kupunguza tatizo la ajira kwa vijana wengi hapa nchini ”.
Akizungumzia
sanaa yake msanii Hilimali alibainisha kuwa hapo awali alikuwa dansa maarufu wa
muziki wa bolingo alipokuwa mdogo na mara nyingi alijishindia zawadi mbalimbali
kama Biskuti, Soda na Pipi zilizokuwa zinaandaliwa kama zawadi kabla ya
kujitumbukiza rasmi katika muziki wa kizazi kipya.
Pia
msanii Hilimali amemtaja mama yake mzazi Bi. Antonia Malundo maarufu kama
mama Maniponela ambaye alikuwa mcheza
ngoma za asili maarufu miaka ya tisini katika wilaya ya Kilosa ndiye
aliyemvutia kujiiingiza katika sanaa ya muziki, ndio maana hata muziki wake
anaoufanya una vionjo fulani vya asili tofauti na wanamuziki wengine wa muziki
wa kizazi kipya.
Pamoja
na hayo Hilimali amebainisha kuwa vikwazo anavyokutana navyo kwenye ufanyaji
wake wa kazi za muziki ni kukosa sapoti ya kutosha kutoka kwa wadau wa muziki ambao mara nyingi wamekuwa
wakiweka mbele maslahi yao binafsi pasipo
kumjali msanii.
Vilevile
msanii huyo ametoa wito kwa serikali kuiwekea mkazo ahadi ya rais ya kulinda
haki za wasanii kwani kwa mfumo ulivyo sasa hapa nchini inakuwa vigumu msanii
kunufaika na jasho lake.
Msanii
Hilimali alianza muziki akiwa darasa la nne mwaka 1995 alipokuwa anakaa na bibi yake wilaya ya
Kilosa sasa hivi inatambulika kama wilaya ya Gairo kata ya Iyobo tarafa ya
Chakwale kijiji cha Makuyu na matarajio yake ni kuwa msanii wa kimataifa.
MASHABIKI WA YANGA WATOA MAONI KUHUSU MCHEZO WA YANGA NA AZAM FC
Na:
Fadhila kizigo
Mashabiki
wa klabu ya Yanga wa mkoani Morogoro wametoa maoni yao kuhusu mchezo wa Ngao ya
jamii dhidi ya Azam FC baada ya Yanga kufungwa kwa jumla mikwaju ya penati 4-1.
Akizungumza
na SUAMEDIA Hassani Yanga amesema kuwa wachezaji wa Yanga imeonekana kulidhika
na magori ya mapema hivyo kubweteka nakuruhusu upande wa wapinzani kuja juu hivyo kuwawia
vigumu kumaliza vema katika dakika za lala salama.
Ameongeza kuwa mchezo ulianza vizuri kwa
kufanikiwa kufunga goli la kwanza kwa mkwaju wa penti ambapo gori lilifungwa na
Donard Ngoma dakika ya 20 na kupata goli la pili dakika ya 21 ya mchezo.
Pia
Bwana Hassani ametoa wito kwa mashabiki wa
Yanga kutokukata tamaa kwakuwa siku zote
matuta huwaga hayana mwenyewe kwaiyo yeyote anaweza kufunga na ndicho kilichotokea tukakosa penati mbili na
wapinzani kupata penati mbili.
Aidha
Farid Mohammed alisema kuwa timu hiyo inahitaji mabeki wa kutosha na mechi
nyingi za kimataifa kupata uzoefu katika kuimarisha timu na wapinzani wajipange
kwa msimu unaoanza kwani kushindwa kwa mechi dhidi ya Azam si kipimo kwao.
NEYMAR AIPA NGUVU TIMU YAKE KUFUZU MASHINDANO YA OLYMPIKI
Na:Adam
Ramadhan
Mshambuliaji wa klabu ya Barcelona
na timu ya Taifa ya Brazil Neymar Junior
ameisaidia timu yake ya taifa kufuzu
fainali katika michuano ya
Olimpiki inayoendelea kufanyika nchini Brazil.
Neymar amefunga
goli la mapema sekunde ya 14 na
kuweka historia ya kuwa goli la mapema zaidi
katika michuano hiyo huku akifunga goli lingine dakika ya 90, Gabriel Jesus
akafunga mara mbili, Marquinhos na Luan pia na kukamilisha idadi ya
magoli 6-0 dhidi ya Honduras.
Manchester
City Gabriel Jesus akafunga mara mbili, Marquinhos na Luan wakafunga pia
kabla ya Neymar kuhitimisha mvua hiyo ya magoli kwa bao lake la dakika za lala
salama kwa mkwaju wa penati.Brazil
itakutana na timu kati ya Nigeria au Ujerumani kwa upande wa wanaume.
Wakati
huohuo Bingwa wa mbio za mita 3000
kuruka viunzi na maji kutoka Kenya Ezekiel Kemboi amenyang'anywa medali yake ya
shaba aliyoishinda mjini Rio de Janeiro, Brazil.
Hata
hivyo Ufaransa ilikataa rufaa baada ya kubainika kuwa mwanariadha huyo alikanyaga nje ya mstari wakati akishiriki
mbio hizo Jumatano kuruka kiunzi na maji.
YANGA YAPOTEZA MCHEZO NGAO YA HISANI DHIDI YA AZAM FC
Na:Adam
Ramadhan
Mabingwa
watetezi wa ligi kuu Tanzania bara klabu ya Yanga imepoteza mchezo wa ngao
ya hisani dhidi
ya Azam FC kwa changamoto ya mikwaju ya penati ,ukiwa ni mchezo wa
ufunguzi wa ligi kuu ya vodacom inayotarajiwa kuanza Jumamosi ya Agosti 20, 2016.
Mshambuliaji
wa Yanga Mzimbabwe Donald Ngoma alifunga bao la kwanza dakika ya 20 ya kipindi cha kwanza kwa njia ya penati
baada ya kuangushwa ndani ya eneo la hatari na beki wa Azam David Mwantika.
David
Mwintika anafanya tena makosa yanayosababisha Yanga kupata goli la pili kwa
kushindwa kuumiliki mpira vizuri, ambapo Amisi Tambwe anachukua mpira na
kumpasia Donald Ngoma na kuweka mpira wavuni
dakika ya 22.
Dakika ya 74 ya kipindi cha pili Shomari Kapombe aliipatia Azam bao la kwanza
akitumia makosa ya mabeki wa Yanga walioshindwa kuondosha mpira kwenye eneo la
hatari la goli lao.
Dakika
ya 90 John Bocco anaisawazishia Azam FC goli la pili kupitia mkwaju wa penati
baada ya beki wa Yanga kushika mpira ndani ya eneo la hatari,penati hiyo ambayo
ilifanya matokeo kuwa 2-2 hali iliyopelekea kupigwa kwa mikwaju ya penati
ambapo Yanga walipoteza mchezo huo.
Penati
za Azam ziliwekwa wavuni na John Bocco,Himid Mao, Michael Balou na Shomari
kapombe,huku penati ya Yanga ikifungwa na Deogratius Munishi pekee.
///////////////////////////////////////////////////////////////////////////////////
//////////////////////////////////////////////////////////////////////////////////
KITENDAWILI NANI ZAIDI YANGA AU AZAM KUTEGULIWA LEO
Na: Adam Ramadhani
Mchezo
wa ngao ya jamii kati ya Yanga dhidi ya Azam utapigwa leo Jumatano Agosti
17,2016 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam
majira ya saa 10:00 jioni ikiwa ni ishara ya ufunguzi wa msimu mpya wa ligi kuu
Tanzania
bara.
Kuelekea
mchezo huo SUAMEDIA imezungumza na baadhi ya wadau wa soka mkoani Morogoro na kusema
kuwa mchezo huo utakuwa mgumu kwa timu zote kutokana usajili uliofanywa na
vilabu hivyo.
“Mimi
naipa nafasi Yanga kutokana na kiwango kizuri walichokionesha katika mchezo
uliopita dhidi ya Mo bejaia” alisema Shukuru Omary mkazi wa Mafiga. Naye Hussein Rajabu shabiki
wa Simba amesema kuwa mchezo huo utakuwa mgumu kutokana na usajili wa klabu
zote mbili.
Hata
hivyo klabu ya Yanga itawakosa wachezaji wake watano akiwemo golikipa Ally
Mustafa, mabeki Kelvin Yondani, Juma Abdul, Andrew Vincent na kiungo
mshambuliaji Obrey Chirwa kutokana na matatizo mbalimbali yanayowakabili ikiwemo
majeraha.
Mshambuliaji
Donald Ngoma anatarajiwa kuwepo katika mchezo wa leo baada ya kukosekana katika
mchezo uliopita wa shirikisho dhidi MO Bejaia kutokana na kadi mbili za njano
alizopata katika michezo iliyopita.
RIADHA
KUFUKA MOSHI LEO KATIKA VIWANJA VYA RIO DE JENEIRO
Na: Adam Ramadhani
Michezo
ya Olimpiki kwa upande wa riadha itaendelea tena leo Agosti 17, 2016, Rio de
Jeneiro nchini Brazil ambapo
wanariadha kutoka nchini Kenya na Uganda
watayawakilisha mataifa yao.
Timu
ya taifa ya riadha ya Kenya
itawakilishwa na wanariadha wake watatu Kipruto Conseslas, Ezekiel Kemboi na
Brimin Kiprop huku timu ya taifa ya Uganda
ikiwakilishwa na Jacob Araptany katika mbio za mita 3000 za kuruka vihunzi.
Lakini
Kenya
imeendelea kung’ara katika michuano hiyo
baada ya usiku wa jana mwanariadha Faith Kipyegon kunyakua dhahabu ya tatu kupitia mbio za mita
1500 kwa wanawake, wakati kwa upande wa wanaume mjamaica Mc Leod alinyakuwa medali
ya dhahabu kupitia mbio za mita 110.
CHELSEA YAIKUNG'UTA WESTHAM UNITED 2-1
Na: Adam Ramadhani
Mechi za
mzunguko wa kwanza wa ligi kuu ya
England zimekamilika usiku wa Agosti 15 ,2016 mara baada ya Chelsea kuwafunga Westham
United magoli 2-1 katika dimba la
Stamford bridge ,ikiwa chini ya kocha mpya Antonio Conte.
Chelsea walikuwa wakwanza kupata
goli kupitia kwa Edern Hazard kwa mkwaju
wa penati dakika ya 47 mara baada ya Cesar Azplicueta kufanyiwa madhambi ndani
ya eneo la hatari,Diego Costa aliipatia Chelsea goli la pili dakika ya 89,huku
goli la Westham United likifungwa na James Collins dakika ya 77.
Kiungo mpya wa Chelsea Ngolo
Kante aling’ara katika mchezo huo akishirikiana vyema kabisa na viungo wenzake
kama Nemanja Matic, Edern Hazard na Emboaba Oscar,Chelsea wanaonekana kuleta
ushindani katika ligi hiyo kutokana na soka safi la mashambulizi na kumiliki
mpira katika mchezo wa jana.
Ligi kuu nchini England
itaendelea tena ijumaa ya wiki hii kwa mchezo mmoja kuchezwa ambapo Manchester united
watakapowakaribisha Southampton majira
ya saa 4:00 usiku katika uwanja wa Old Trafford.
LIGI KUU YA ENGLAND YAENDELEA TENA LEO
Na: Adam Ramadhani
Ligi kuu ya nchini England
itaendelea tena leo Jumatatu Agosti 15,2016,ambapo Chelsea watawakaribisha Westham United katika dimba
la Stamford Bridge majira ya saa 4:oo usiku.
Tayari michezo 9 imechezwa
jumamosi na jumapili ya wiki iliyopita,mabingwa wa msimu uliopita Leicester
city wameanza vibaya ligi hiyo mara baada ya kukubali kipigo cha
magoli 2-1 kutoka kwa hully city,Crystal Palace walikubali kipigo cha goli 1-0
kutoka kwa Westbrom Albion huku
Swansea 1-0 wakiwafunga vijana wapya wa ligi hiyo
Middlesbrough ,Manchester city ikiifunga Sunderland 2-1.
Klabu ya Southampton ilikubali
sare ya 1-1 dhidi ya Watford, Tottenham ikibanwa mbavu ya suluhu ya 1-1 kwa
Everton,huku Burney ikilizamisha sare ya goli 1-1 dhidi Stoke city,Manchester
united inayonolewa na kocha mpya Jose Mourinho iliibuka na ushindi wa jumla ya magoli 3-1
dhidi ya AFC Bournemouth.
Arsenal ilipoteza mchezo wa kwanza dhidi ya
Liverpool kwa jumla ya goli 4-3
,Arsenal imekubali kichapo cha magoli manne kwenye mchezo wa ligi
kwa mara ya kwanza tangu M\ay 2009
ilipochapwa na Chelsea jumla ya magoli 4-1.
0 Comments