SUAMEDIA

HABARI






 MAFUNZO YA KUENDESHA MITANDAO KUZAA MATUNDA (SUA)



Na: Alfred Lukonge na Tatyana Celestine

Mafunzo kwa waendesha mitandao kutoka Vitivo, Idara, na Vituo mbalimbali vya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) yanaendelea tena leo katika Kampasi ya Mazimbu ikiwa na lengo la kuwaongezea weledi wa kusambaza taarifa za chuo kwa uraisi kwenye tovuti zao.
Mwezeshaji wa mafunzo Bwana Kundasen Swai akitoa mafunzo jana katika Kampasi ya Mazimbu mkoani Morogoro

Akitoa mada mmoja wa wawezeshaji wa mafunzo hayo Bw. Kundasen Swai amebainisha kuwa ili tovuti ipate watembeleaji wengi ni muhimu kuangalia ubora wa taarifa unazituma ili watu duniani wapate kuzisoma.

Natoa wito kwa kila Idara chuoni SUA kuwa na tovuti yake na kuhakikisha tovuti hizo zinakuwa na wasifu wa kila mfanyakazi wa idara hiyo kwani kwa kufanya hivyo nafasi ya chuo duniani itapanda pamoja na kuongeza wanafunzi pia kukitangaza chuo kwa uwanda mpana”.alisema Swai


 Kwa upande wao washiriki waliohudhuia mafunzo hayo walitoa maoni yao ni kwa jinsi gani wamefaidika na mafunzo vilevile mategemeo yao baada ya kumaliza mafunzo yao. 

Nae Bi Inosencia  Nyanghura alisema kuwa kikubwa ni kupata weledi kila kitu kinaweza kufanyika kwa uhakika.

"masuala ya tovuti nilikuwa  naona ni ya watu wenye ujuzi wa Teknolojia ya Mawasiliano pekee lakini baada ya mafunzo haya nimeona vitu ni virahisi na mtu yeyote anaweza kuvifanya" alisema Nyanghura.

 Kwa upande wake Bwana Christian Paul ameeleza kuwa imekuwa ni rahisi kwa sasa baada yakupata mafunzo kwani vikwazo ambavyo vilikuwa vinawasumbua haviakuwapo tena.

 "matatizo yalikuwa yakitutokea tulilazimika kuwafuata watu wa kituo cha komputa lakini kupitia mafunzo haya sasa nitaweza kutatua matatizo ya kimtandao mimi mwenyewe" alisema Paul.

Semina hiyo imeandaliwa na Kituo cha Kompyuta chuoni SUA na inategemewa kufungwa siku ya Jumatano ya tarehe 31/8/2016 huku washiriki wakitegemewa kutoka na mbinu za kupandisha nafasi ya chuo duniani kwa njia ya mtandao.


 

 

UNYWAJI WA MAZIWA YASIYOCHEMSHWA KUSABABISHA MAGONJWA: PROF. KAZWALA




Rebeka Nyaulingo

Imeelezwa kuwa unywaji wa maziwa ambayo hayajachemshwa kuna uwezekano mkubwa wa kupata vimelea vya magonjwa mbalimbali kutoka kwa mnyama kwenda kwa  binadamu.
 
PROF RUDOVIC KWAZWALA KUSHOTO

Akizungumza na Suamedia ofisini kwake Profesa Rudovick Kazwala amefafanua kuwa maziwa mabichi yanavimelea mbalimbali vya wadudu ikiwa ni Tb pamoja na bluselasi ambapo humfanya binadamu kupata homa za mara kwa mara na wakati mwingine ugonjwa  na kushindwa kuendesha maisha ya kila siku.


Aidha Prof Kazwala amesema kuwa magonjwa haya ambayo yanatokana na wanyama mara nyingi yanapoingia kwenye mwili wa mwanadamu humfanya mtu kupata homa za mara kwa mara na kukosa nguvu kazi ya uzalishaji mali na kushuka kiuchumi  kwa taifa.

Wakati huo huo Prof Kazwala amefafanua kuwa vimelea hawa wa Bluselasi na Tb wamefanikiwa kuwashambulia zaidi jamii ya wafugaji katika maeneo ya kilosa, Mvomero, Manyara, Kiteto, pamoja na Arusha kutokana na kutochemsha maziwa kwa ufasaha.

Hata hivyo watu wa jamii zote wanatakiwa kuwa makini na afya zao kwa kujali kuchemsha maziwa kwa umakini zaidi kwa lengo la kuondokana na magonjwa yanayoambukizwa kutoka kwa mnyama kwenda kwa binadamu.





NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI ZATEGEMEA MALIGHAFI KUTOKA NJE

Rebeka Nyaulingo

Imeelezwa kuwa nchiza Afrika Mashariki zimekuwa na uzalishaji mdogo wa malighafi nahivyo zimejikuta zikitegemea nchi za bara la Ulaya pamoja na China jambo linalopelekea kudumuza uchumi wake.
PICHA NA MTANDAO



Akizungumza na Sumedia na wadau mbalimbali wanaojihusisha na  uchumi Profesa Joseph Hella amebainisha kuwa halihiyoinatokananauhafifu wa miundombinu yauzalishaji wa bidhaa na hasa viwanda.

Aidha  Profesa Hela amebainisha kuwa kutokana na uhafifu wa miundombinu ya uzalishaji wa bidhaa ndio unaosababisha nchiza Rwanda, Kenya, Uganda, Tanzania  na Uganda  kuwa ni watu wa kupokea zaidi kuliko kutoa na hilo amesema  kuwa katika ushindani wa kukua kwa masoko China ipo juu kuliko nchi za bara la Ulaya .
Profesa Hella kwa sasa anafanya utafiti wa zao la pamba isiyotumia dawa wala mbolea katika Wilaya ya Meatu ,Maswa, Saranda Dodoma ,Mbeya, Mtwara pamoja na Shinyanga utafiti unaoweze kuwanufaisha wakulima.
 

 

WAKAZI WA MOROGORO WATOA MAONI YAO KUHUSU MAZOEZI YA POLISI




Baadhi ya Wakazi wa Manispaa ya Morogoro wametoa maoni yao kuhusu kitendo cha jeshi la polisi hapa nchini  kuwa katika mazoezi makali ya kijeshi yanayoendelea nchi nzima. 



PICHA NA MTANDAO



Wakizungumza na SUAMEDIA Bw. Sadiki Ramadhani na Bw. Godfrey Mlay wakazi wa Tumbaku Mjini Morogoro wamebainisha kuwa mazoezi yanayofanywa na polisi yanawatia hofu ya kutokea mapambano kati ya polisi na vyama pinzani yaani UKAWA.

Wamesema kuwa mazoezi haya ya kijeshi yanayoendelea yanawapa hofu na kudhani kuwa kukawa na mapambano makali baina ya pande hizo mbili siku ya tarehe moja mwezi wa tisa kama yalivyoandaliwa na kutangazwa Vyama vya upinzani nchi nzima.

Kwa upande wake Bi. Tatu Shomari mkazi wa Mafiga Mjini Morogoro amesema kuwa watu wasijenge hofu kwani mazoezi yanayoendelea inasemekana nikatika kuimarisha jeshi lapolisi na sio maandalizi ya kupambana na kitu chochote za kisiasa.

 

 

WAKULIMA WAMETAKIWA KUTUMIA MBEGU  ZA MAHINDI ZINAZOSTAHIMILI UKAME


Na.Suzane Cheddy.

Wakulima nchini wametakiwa kutumia mbegu bora za mahindi  zilizofanyiwa utafiti na mbazo zimewekewa uwezo wa kukabiliana na changamoto ya ukame ili kumhakikishia mkulima kupata mazao bora badala ya kutumia mbegu za asili mbazo hazina uwezo huo na kusababisha mkulima kupata hasara kila mwaka.





Wito huo umetolewa na Mtafiti mkuu kiongozi kutoka  tume ya taifa ya sayansi na teknologia ( COSTECH)  Dr.Nicholas Nyange wakati akiongea na SUA MEDIA juu ya mafanikio yaliyopatikana katika kuzalisha mahindi chotara yanayostahimili ukame kupitia mradi wa WEMA.


 Amesema ukame ni tatizo kubwa linalokumba maeneo mbalimbali ya Tanzania na nchi jirani ndio maana Mradi huo unashirikisha pia watafiti wan chi nyngine ambazo ni Uganda,Kenya,Msumbiji ,afrika ya kusini na washirika wa kimataifa katika kutafuta teknolojia itakayoweza kumsaidia mkulima wa mahindi kulima kilimo chenye tija na kumuondoa kwenye hasara kila mwaka.

Dr. Nyange amesema Utafiti huu ulianza mwaka 2009 kwa lengo la kutafuta mbegu chotara ambazo zinaweza kustahimili ukame na mpaka sasa mradi huo  imefanikiwa kupata aina sita ya mbegu zinazostahimili ukame huku  aina nne kati ya hizo  zimeidhinishwa  na waziri wa kilimo,uvuvi na mifugo kwa ajili ya kupelekwa sokoni.

Mtafiti huyo kiongozi toka COSTECH  ameongeza  kuwa utafiti umeweza kuleta mafanikio makubwa kwa wakulima walioanza kutumia mbegu hizo za mahindi  zinazostahimili ukame.


 

 

 

SUAMEDIA KUPONGEZWA KWA KAZI WANAYOFANYA MKOANI MOROGORO

 Na: Ayub Mwigune

Wadau mbalimbali wa Manispaa ya Morogoro wamesifu kazi nzuri inayofanywa na SUAMEDIA katika kutoa elimu mbalimbali hususani kilimo, kuburudisha na kusaidia jamii kupitia vyombo vyake vya habari.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwa nyakati  na mwandishi wa habari hii wamesema wamekuwa wakifuatilia habari zinazo andikwa kwenye blog ya SUAMEDIA zimewafanya wawe mstari wa mbele katika kuata habari zinazoendana na wakati.

Christian Jawadu ambaye ni Mkazi wa Mafiga amesema yeye ni mfuatiliaji sana wa habari zinazo andikwa na SUAMEDIA na amewapongeza wandishi wa habari wa kituo hicho kwa kuandika habari ambazo zimekuwa za kweli na uhakika pia amewaomba waweze kufungua kurasa za mitandao ya jamii kama facebook na twiter iliwa waweze kufikia jamii kubwa  ya vijana wanaotumia kwa wingi mitandao hiyo.

Naye Ramadhan Daraja amewasifu SUAFM kwa nyimbo mbalimbali ambazo zimekuwa zikichezwa na kituo hicho kwani zimekuwa zikilenga makundi mbalimbali ambayo yapo katika jamii kama vile vijana, wazee pamoja na waumini wa dini hivyo kufanya jamii kuburudika na kuelimika kupitia kituo hicho.

Naye mwanamziki wa bongofleva  Hanset Wyclef maarufu kama Hansreal amesema uwepo wa SUAFM utasaidia kukuza na kuinua vipaji vya wasanii wachanga nchini Tanzania  kwani imekuwa ni vigumu nyimbo zao kuchezwa radio nyingine lakini SUAFM imekuwa haina ubaguzi huo hivyo imetoa wito waendelee  kufanya vizuri ili kukuza muziki wa Tanzania hususani kusaidia wasanii wachanga waweze kupata nafasi ya kusikika nyimbo zao.

 


 WANANCHI WAIOMBA SERIKALI KUSHUGHULIKIA MTO KIKUNDI MOROGORO

Na: Lucy Mndeme
  Wananchi wanaoishi kando kando ya mto Kikundi unaopita katikati ya Manispaa ya Morogoro, wameiomba serikali ya mkoa huo kutafuta uwezekano wa kuuchepusha, ili usipite katikati ya mji.
Baadhi ya wananchi hao wameiambia SUAMEDIA kuwa mto huo ambao wakati wa kiangazi hukauka, umesababisha kuwepo kwa madaraja mengi katikati ya mji.
Mmoja wa wananchi hao Juma Mohamed Mkambi amesema mto Kikundi una madaraja zaidi ya matano kutokana na kupita katikati ya manispaa  ya Morogoro.
Amesema kutokana na gharama kubwa za kuhudumia madaraja hayo, mto huo ungeweza kuchepushwa na kupita eneo la Chuo cha Mifugo LITI na kuingia mto Morogoro, hivyo kuondoa usumbufu wa kuhudumia madaraja ambayo hayana tija kwa wananchi.

Mkambi amesema mto huo ambao maji yake si safi na salama, hautoi huduma yoyote kwa wananchi wanaoishi kandokando ya mto huo, zaidi ya kugeuzwa dampo la taka ngumu na maji taka kufuatia baadhi ya wakazi waliojenga kando ya mto huo kuelekeza maji ya vyooni kwenye mto huo.
Naye mwananchi mwingine aliyeomba jina lake kuhifadhiwa aliiomba idara ya afya Manispaa ya Morogoro kuwazuia wakulima wadogo wa mboga za majani kutumia maji hayo kunyweshea bustani zao, kutokana na maji hayo kuwa na kila aina ya uchafu, hivyo kuhatarisha maisha ya watumiaji wa mboga hizo.


 

KILO 370 ZA NYAMA POLI ZAKAMATWA  KIJIJI CHA BWAKILA MOROGORO VIJIJINI


Jeshi la Polisi mkoani Morogoro linamshikilia mtu mmoja baada ya kumkuta na nyamapori kilo 370 katika kijiji cha Bonye  Tarafa ya Bwakila Wilaya ya Morogoro vijijini.
 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro akionesha dhana zilizokamatwa zinazotumika kuulia wanyama pori

Tukio hili limetokea  mnamo tarehe 19 augost mwaka huu majira ya saa3:30 asubuhi.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Mkoani Morogoro Ulrich Matei amesema tukio hilo limetokea Jumamosi Agosti 19 saa 3.3 asubuhi na kuwa  mtuhumiwa huyo ambae anajulikana kwa jina la Koba Nasibu alikutwa na nyama ya Pundamilia Kg 260, Nyumbu kg 50, Swala kg 40 pamoja na nyama ya Ngiri kg 20.

Aidha kamanda Matei amesema kuwa mtuhumiwa huyo amekamatwa na viungo mbalimbali vya wanyamapori hao ikiwa ni mikia miwili ya pundamilia, pembe mbili za nyumbu, pamoja na pembe mbili za swala.

Hata hivyo kamanda Matei amesema thamani ya nyama na viungo vya wanyamaori hao bado haijafahamika.





WAFUGAJI WAMPIGA HADI KUFA MKULIMA WILAYANI KILOSA


Na:Ashura Janati 

Kijana mmoja Mkazi wa Kijiji cha Tindiga Wilaya ya Kilosa amefariki dunia baada ya kupigwa na wafugaji wa kimasai waliokuwa wakilisha mifugo yao shambani kwake.

Diwani wa kata ya Tindiga Mhe. Yahya Mbaruku Mbachi amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo na kumtaja kijana aliyeuawa kuwa ni Ali Mbaruku Makakala  na tukio hilo limetokea tarehe 16 Agosti majira ya mchana.

Mhe. Mbachi amesema taarifa ilifika kijijini kuwa wafugaji hao wa kimasai walikuwa wakilisha mifugo yao katika mashamba ya wanakijiji, na marehemu Makakala na vijana wengine ambao ni polisi jamii wa kijiji hicho walikwenda kuhakiki ukweli wa taarifa hizo.

Amesema walipokaribia eneo walipokuwa wakilisha mifugo hiyo marehemu alibaini kuwa ng’ombe hao wako shambani kwake ndipo alipokimbia kuelekea huko na kuwaacha nyumba vijana wenzie lakini akashambuliwa na wafugaji hao kusabababisha kifo chake papohapo na wafugaji hao wakatokomea na ng’ombe zao.

Kufuatia hali hiyo wananchi wa kijiji cha Tindiga waligoma kumzika marehemu wao hadi mkuu wa wilaya ya Kilosa afike eneo la tukio na imeelezwa baadaye mkuu huyo wa wilaya ya Kilosa alifika na kuagiza kuheshimiwa kwa mipaka kati ya Tindiga kwa wakulima na Mkata ndio kwa wafugali eneo linaloitwa Samunge.

Juhudi za jeshi la polisi zinaendelea kuwasaka watuhumiwa hao ni mkondo wa sheria ufuate.




WANANCHI WA LUKOBE KUKAIDI AGIZO LA MKURUGENZI WA MANISPAA


Na: Mazoea Iddy


Wananchi wa Kata ya Lukobe Manispaa ya Morogoro wameendelea kufanya shughuli zinazodaiwa kusababisha uharibufu wa mazingira katika kingo za mto Ngerengere licha ya kupewa notisi 




Akizungumza na SUAMEDIA Afisa Mtendaji Kata ya Lukobe Bw. Selemani Mjata amesema kuwa zuio lililotowa mnamo 25/11/2015 kukataza kufanya shughuli yoyote ambayo itaweza kuharibu kingo za mto huo lakini wananchi hao bado wamekaidi agizo hilo.


Aidha kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtaa wa Tuelewane Bw. Ally Mohamedi Gwandu ameeleza kuwa wananchi hao bado wanaendelea kufanya shughuli za kilimo cha mboga mboga na ufyatuaji wa matofali.


Ameongeza kuwa Viongozi wa Mtaa wamejipanga kwa dhati ikiwezekana kutumia vyombo vya dola ili kuwaondoa katika maeneo hayo hatarishi kwa mazingira


 Aidha wananchi wa Kata wameiomba serikali kuwatafutia sehemu halali ya kufanyia shughuli hizo ili kuhepusha uharibifu wa mazingira kwani wanalazimika kufanyia eneo hilo kwa kujiingizia kipato.


 

TEMBO AVAMIA KIJIJINI NA KUUA MTU MMOJA

Na: Mazoea Iddy      

Mnyama aina ya Tembo amevamia katika Kijiji cha Kilangalimkata Tarafa ya Kimamba Wilaya ya Kilosa Mkoa wa Morogoro na kusababisha mauaji ya Samson Jakob mwenye umri wa miaka 35 ambaye ni Mkazi wa Kijiji hicho.




Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro ACP Leonce Rwegasira alisema kuwa tukio hilo limetokea mnamo tarehe 12/08/2016 majira ya saa saba usiku.


Taarifa zinasema kuwa, Tembo huyo alivamia kibanda shambani kwa marehemu akiwa amelala na kukivunja ambapo marehemu alifariki dunia mara baada ya kukanyagwa na Tembo sehemu mbalimbali za mwili wake. 


Aidha Jeshi la Polisi limesema kuwa linaendelea na uchunguzi juu ya tukio hilo.
 

 

MWANAMKE AKUTWA AMEKUFA HOTELINI KILOSA MKOANI MOROGORO



Na: Ashura Janati


Mwanamke mmoja anayekadiriwa kuwa na  umri  wa miaka 38 anayejulikana kwa jina la Mwajabu  Kilosound  Mkazi wa Kilosa Mjini mkoani Morogoro  amekutwa amefariki dunia akiwa hotelini mjini Kilosa.


Tukio hilo liligunduliwa siku ya Jumapili agosti 14 kunako saa 5 asubuhi  baada ya mhudumu wa hoteli hiyo  kumkuta marehemu akiwa katika chumba alicholala na kutoa taarifa kwa mmiliki wa hoteli hiyo.



Akizungumzia  kifo hicho Kaimu Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Kilosa aliyefika katika eneo la tukio Eusebio Nyalifa amesema ukaguzi wa awali unaonyesha kuwa marehemu amefariki  dunia akiwa hana jeraha lolote mwilini mwake.





Kwa mujibu wa watu waliokuwa karibu na marehemu Mwajabu waliielezea SUAMEDIA kuwa katika siku za karibuni  alikuwa na mahusiano na mwanaume ambaye alikuwa mgeni katika eneo hilo na baada ya tukio hilo mwanaume huyo alitoweka na hadi sasa haijulikani alipoelekea.



Nao watoto wa marehemu  wamesema kuwa mwanaume huyo alikwenda asubuhi katika duka lao la vinywaji  na kuwaambia yeye na mama yao wanasafiri hivyo wampe fedha za mauzo ya dukani na kuongeza kuwa waendelee na ratiba zao za kila siku.



Jeshi la polisi likishirikiana na wananchi linaendelea kumtafuta  kijana huyo aliyekuwa na marehemu katika hoteli  hiyo.

 


              BW. MRISHO GAMBO KUWA MKUU WA MKOA WA ARUSHA


 RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amefanya mabadiliko madogo ya uongozi na kumteua Bw. Mrisho Gambo kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha kuanzia leo (Alhamisi, Agosti 18,2016).
Mkuu wa Mkoa mpya wa Arusha,Mrisho Gambo aliyeteuliwa na Rais,kuapishwa kesho ijumaa Ikulu jijini Dar


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Bw. Gambo anachukua nafasi ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo, Bw. Felix Kijiko Ntibenda ambaye uteuzi wake umetenguliwa.


Amesema Bw. Ntibenda anahamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu ambako atapangiwa majukumu mengine.

Kabla ya uteuzi huo, Bw. Gambo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha. Ataapishwa kesho (Ijumaa, Agosti 19, 2016) saa 3 asubuhi Ikulu jijini Dar es Salaam.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S. L. P. 3021,
11410 DAR ES SALAAM.





          UNYANYASAJI WA KIJINSIA WALETA ATHARI ZA KISAIKOLOJIA SUA


Na: Consolata philemon


Madhara ya Unyanyasaji wa Kijinsia yameonekana kuleta athari kubwa kisaikolojia, kimwili na kupelekea kupungua kwa tija uande wa wafanyakazi na kushuka kwa kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi.




Hayo yamesemwa na Dokta Sotco Komba alipokuwa akitoa mrejesho kuhusu utafiti wa Unyanyasaji wa Kijinsia kwa wafanyakazi na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo katika  hafla ya uwasilishaji matokeo ya utafiti iliyofanyika chuoni hapo.

Dkt Komba amesema malengo ya utafiti huo ni kuwezesha kupatikana kwa uelewa wa kina kuhusu hali na ukubwa wa tatizo la Unyanyasaji wa Kijinsia chuoni SUA  na kutoa mapendekezo ya namna bora ya kikabiliana na tatizo hilo.

Kadhalika Dkt Komba  amesema baadhi ya mambo yanayopelekea kuwepo kwa unyanyasaji wa kijinsia ni pamoja na tabia binafsi  za watu, mavazi yanayoshawishi, kiwango kidogo cha mikopo na kuchelewa kwa fedha  ya chakula  kutoka bodi ya mikopo, na uwepo wa wafanyakazi wengi wasiofahamu haki na kanuni za kazi zilivyo.

Pia Dkt Komba amefafanua zaidi kuwa utafiti huo umebaini madhara ya kisaikolojia  yameonekana kuwa na asilimi 94.4 , madhara ya kimwili ni asilimia 5.6  huku watekelezaji wa vitendo vya unyanyasaji wa  kijinsia ni wanafunzi wa kike asilimia ambao wanavaa nguo zisizo na staha kwa asilimia 34.3  wanafunzi wa kiume kwa asilimia 31.5 na wanataaluma wa kiume kwa asilimia 15.4 wakati wa mafunzo kwa vitendo.

Upande wa wafanyakazi waliohudhuria katika hafla hiyo Bw.Erasto Mnyatu amewaomba watafiti hao kuweka mapendekezo kwa Chuo kuunda chombo huru chenye uwazi cha kusimamia  matatizo ya kesi za unyanyasaji wa kijinsia  ndani ya  taasisi.

Utafiti wa  unyanyasaji wa kijinsia kwa wafanyakazi na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo umefanywa  na Profesa Aida Isinika  na Dkt Sotco Komba chini ya kamati ya Chuo  inayojihusisha na utekelezaji  wa sera ya jinsia (GPIC) na kitengo cha Jinsia katika mradi wa iAGRI lengo likiwa ni kujua hali ya tatizo hilo hapa SUA.



MTU MMOJA MKOANI MOROGORO ASHIKILIWA KWA TUHUMA ZA ULAWITI


Na: Fadhila Kizigo 
   
Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro linamshikiria mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Alhaj Hussen Doto [27] mkazi wa sabasaba kwa tuhuma za kuwalawiti watoto wawili majina yanahifadhiwa.



 
Akizungumza na Waandishi wa Habari kaimu  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro ACP Leonce Rwegasira amesema kuwa mnamo Agosti 13 mwaka huu majira ya saa tano usiku maeneo ya Uwanja wa Taifa manispaa ya Morogoro, mama wa mtoto mmojawapo aligundua kuwa mtoto wake wa miaka mitatu amelawitiwa.

Kamanda Rwegasira amesema mama wa mtoto huyo aligundua baada ya mtoto kulalamika kuwa na maumivu makali sehemu yake ya siri yeye na mtoto mwenzie jina linahifadhiwa mwenye umri wa miaka [5] wote ni majirani na wakazi wa uwanja wa taifa.

Ameeleza aliwagundua kuwa wamefanyiwa kitendo hicho  na baada ya kuwadadisi watoto hao walimtaja mtuhumiwa aliyewatendea kitendo hicho ambaye ni Alhaji Hussen Dotto.

Kamanda Rwegasira amesema kuwa watoto wanaendelea na matibabu katika hospital ya rufaa mkoa wa Morogoro pia mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa na atafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika. 



   VYETI BANDIA ZAIDI YA 1000  VYANASWA



Sehemu ya vyeti bandia zaidi ya 1000 kwa ajili ya Taaluma ya uuguzi  ufundi mbalimbali ambavyo vimekamatwa na polisi mkoani Kigoma kwa kushirikiana na maafisa wa Baraza la Wafamasia vyeti ambavyo vilikuwa tayari kugawanywa kwa ajili ya matumizi ya kuwapatia watu ili vitumike kutafutia ajira.
 (Picha na Fadhili Abdallah)

 
                                   

PONGEZI KWA KITUO CHA RADIO SUAFM


Na.Adam  Ramadhan

Wasanii  wa muziki wa kizazi  kipya (Bongofleva na Hip-hop) wametoa  shukrani zao za dhati kwa kituo cha redio cha SUAFM kinachorusha matangazo yake kwa majaribio kutoka mkoani Morogoro  kwa kusapoti  na kupiga Muziki wao.



Wakizungumza na SUAMEDIA  baadhi  ya wasanii  waliofanya mahojiano mafupi  wametoa shukrani zao  kwa  Uongozi na wafanyakazi wa kituo hicho  kwa kuzipiga  bure  nyimbo zao ambazo  wamekuwa wakizileta  kituoni hapo.


Emanuel   Kasolela(27)  aka Pacha B  ni msanii wa Bongo Fleva  amesema kuwa licha ya nyimbo zake kupigwa kwenye kituo cha SUAFM amekuwa akikutana na changamoto kubwa  ya  kipato na sapoti ya nyimbo zake kupigwa kwenye redio.

Kassimu Bochu aka Bochu  amesema kwa chipukizi wanaoanza  muziki inatakiwa wapewe kipaumbele ili waweze kufikia malengo  na hivyo  anaipongeza SUAFM kwa kuzipiga nyimbo zote za wasanii wa Morogoro.

SUAFM ni redio inayorusha matangazo yake kwa majaribio kutoka mkoani Morogoro ikiwa katika masafa ya 101.1 huku ikishika takribani mikoa 10 nchini Tanzania.

Post a Comment

0 Comments