SUAMEDIA

JIFUNZE KILIMO CHA MBOGAMBOGA


Tengeneza tuta la kubwa wa 1m x 2m (ama urefu unaoona wewe kuwa unakufaaa ila tu upana ubaki kuwa 1mita) . Urefu na idadi ya matuta hutegemea kiasi cha mbegu. Kiasi cha mbegu kwa hectare moja ni kilo 6 au 2 kg kwa eka.

Weka samadi iliyooza vizuri kiasi cha debe moja au mchanganyiko wa mbolea ya TSP na CAN (200gm) kwa uwiano wa 1:1 kwenye tuta changanya vizuri na udongo.

Sia mbegu kwenye mistari kwa nafasi ya 1 sm x 20 sm. Tawanya mbegu vizuri wakati wa kusia ili miche isisongamane.

Funika mbegu na weka matandazo ya nyasi kavu juu ya tuta na mwagiliwa maji. Udongo unatakiwa kuwa na unyevu kiasi mpaka mbegu ziote.

Nyasi ziondolewe mara tu mbegu zikiota .

Miche itunzwe vizuri na kitalu kiwe katika hali ya usafi.

Miche imwagiliwe maji mpaka ifikie umri wa kupandikiza shambani.

Sehemu ya kitalu iwe wazi, mbali na kivuli na kiwe karibu na chanzo cha maji.

KUMBUKA:siku za ukaaji wa mbegu kitaruni inategemeana na aina ya mbegu ama zao.

KWA HISANI YA MUUNGWANA BLOG



Post a Comment

0 Comments